Gavana wa chama tawala afurushwa Nigeria

...................



Goodluck Jonathan alichaguliwa kwa mara ya kwanza mwaka 2011
Chama tawala nchini Nigeria kimemsimamisha uwanachama kwa muda gavana mwenye ushawishi mkubwa nchini Nigeria, Rotimi Amaechi, ambaye hamuungi mkono Rais Goodluck Jonathan kuwania tena urais mwaka 2015.
Bwana Amaechi,kutoka jimbo lenye utajiri mkubwa wa mafuta Rivers state, aliteuliwa mwishoni mwa wiki kuwa mwenyekiti wa kikao cha magavana kote nchini.
Lakini mpinzani wake mkuu kutoka jimbo la Plateau, Jonah David Jang, alipinga matokeo ya uteuzi huo na hivyo kujitangaza mwenyewe kama mwenyekiti.
Kawaida Magavana wa majimbo 36 ya Nigeria wana ushawishi mkubwa na wametengewa pesa nyingi kwa ajili ya usimamizi wa majimbo yao.
Mwandishi wa BBC mjini Lagos, Will Ross, anasema kuwa magavana wana ushawishi mkubwa kushawishi wapiga kura kumchagua mgombea fulani katika uchaguzi wa kitaifa.
Bwana Amaechi, mwenyekiti wa sasa wa kikao cha magavana kote nchini alipata kura 19 dhidi ya kumi na sita za mpinzani wake wakati akichaguliwa kwa wadhifa huo. Gavana mmoja hakuhudhuria shughuli hiyo.
Bwana Jang,mwanachama wa (PDP), pia alipinga matokeo ya uchaguzi huo.
Wadadisi wanasema kuwa washirika wa rais wanataka kupunguza ushawishi wa gavana huyo.
Katika mkutano wa dharura wa chama hicho, Jumatatu, maafisa walisema kuwa bwana Amaechi amefurushwa chamani kwa muda kwa kukiuka sheria za chama.

kutoka bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: