Mbowe ataka kujua makampuni yaliyolipa ada - JIBU LA SWALI LA MBUNGE HAI
MBUNGE wa Hai Freeman Mbowe (CHADEMA) ameitaka serikali kutaja
idadi ya makampuni ya mafuta na gesi yaliyolipa ada ya kila mwaka kwa
ajili ya kuwasomesha watanzania katika sekta ya hiyo. “Inaonyesha
makampuni hayo yanatakiwa kulipa Dola 150,000 za Marekani kila mwaka
lakini kuna baadhi ya kampuni hazijalipa ada hiyo mpaka sasa,” alisema
Mbowe. Alihoji
jambo hilo alipouliza swali la nyongeza na alitaka kujua ni kwa nini
serikali isilete wataalamu kutoka nje kuja kuleta elimu ya mafuta na
gesi ili kupunguza gharama. “Gharama
ya dola milioni 6.6 za Marekani kusomesha watu 27 ni kubwa… kwa nini
serikali isione umuhimu kuimarisha kitengo cha jiolojia kilichoko Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam ili kupunguza gharama?” alihoji Mbowe. Akijibu
swali hilo Naibu Waziri wa Nishati na Madini, Stephen Massele, alisema
ana orodha ya makampuni 25 aliyoahidi kumkabidhi mbunge huyo.
Kuhusu suala la gesi alisema kwa sasa Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM)
kina kitengo kinachotoa mafunzo ya mafuta na gesi na kwamba wapo
wanafunzi wanaolipiwa na serikali. Maselle
alisema serikali itaendelea kuongeza bajeti na kutanua wigo katika Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam kupitia kitengo cha Jiolojia ili kupata
wataalamu wengi wa mafuta na gesi. “Ni
kweli gharama inayotumika ni kubwa lakini tayari tumeanza kutoa mafunzo
hayo hapa nchini kupitia baadhi ya vyuo ili kuweza kupata wataalamu
wengi kulingana na umuhimu wa sekata hiyo, pia tutaendelea kuwapeleka
nje ya nchi kwa ajili ya kupata ujuzi zaidi,” alisema.Awali
katika swali la msingi, Mbowe alitaka kujua ni wanafunzi wangapi hadi
sasa wamesomeshwa kwa fedha zinazotolewa na makampuni ya mafuta na gesi
ya TPDC. Kwa
mujibu wa naibu waziri huyo, idadi ya makampuni yaliyoko nchini yenye
mikataba ya utafutaji huo ni 25 ambayo hadi sasa yamechangia kiasi cha
Dola 12,425,000 za Marekani.
chanzo:mtandao.net
0 comments: