Orodha ya matajiri marehemu Hii Hapa

...................

Paul Walker aingia Orodha ya matajiri marehemu

Paul Walker
Mwigizaji nyota wa Fast & Furious Paul Walker ameingia kwenye orodha ya karibuni zaidi ya Forbes ya wasanii marehemu wanaopata pesa nyingi zaidi.
Walker, aliyefariki katika ajali ya barabarani 2013, alijizolea $10.5m (£6.8m) mwaka mmoja uliopita na sasa yumo katika nambari tisa.
Michael Jackson anaongoza kwa mwaka wa tatu mtawalia, akipokea $115m (£75m), ingawa ameshuka kutoka $140m alizojizolea 2014.
Elvis Presley yumo nambari ya tatu $55m (£35.8m), naye aliyetunga filamu ya Peanuts creator Charles Schulz yumo nambari nne na $40m (£26m).
Mzaliwa wa Uingereza aliye kwenye orodha hiyo ni Elizabeth Taylor katika nambari tano.
Hawa hapa ndio wasanii 13 walio kwenye orodha hiyo ya Forbes:
  1. Michael Jackson: $115m (£75m)
  2. Elvis Presley: $55m (£35.8m)
  3. Charles Schulz: $40m (£26m)
  4. Bob Marley: $21m (£13.7m)
  5. Elizabeth Taylor: $20m (£13m)
  6. Marilyn Monroe: $17m (£11m)
  7. John Lennon: $12m (£7.8m)
  8. Albert Einstein: $11m (£7.1m)
  9. Paul Walker: $10.5m (£6.8m)
  10. Bettie Page: $10m (£6.5m)
  11. Theodor Geisel (Dr Seuss): $9.5m (£6.1m)
  12. Steve McQueen: $9m (£5.8m)
  13. James Dean: $8.5m (£5.5m)
chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: