UTATA HABARI ZA MWANA MUZIKI SAIDA KUSEMEKANA AMEFARIKI

...................


saida-karoli
Kuna tetesi kuwa mwanamuziki mashuhuri Afrika Mashariki, Saida Karoli amefariki dunia baada ya kuzama maji kufuatia ajali ya boti iliyotokea kwenye ziwa Victoria. Ajali hiyo ilitokea baada ya boti aliyokuwa akisafiria kutoka Kisiwa cha Goziba kukumbwa na dhoruba na kuzama katika Ziwa Victoria.
Taarifa hizo zinasema pamoja na Saida Kalori, kuna watu wengine pia wamefariki dunia katika ajali hiyo. Idadi ya waliofariki kwenye ajali hiyo bado haijapatikana

chanzo:Gumzo la jiji



Taarifa: Saida Karoli yuko hai. Kweli ajali ya boti imetokea lakini Saida hakuwemo

saida-karoli
Mtandao wa Wavuti unaripoti taarifa ya Neville Meena kuwa ingawa ni kweli kuna ajali ya boti iliyotokea, mwanamuziki Saida karoli hakuwa mmoja wa waliokuwemo kwenye boti hiyo na yuko hai!
Advertisement

Taarifa hiyo imetoa angalizo kutafuta uhakika kwani inasemekana kuwa Saida Karoli ni mzima, yupo jijini Dar es Salaam: “Nimetafuta namba yake ya simu sijaipata, ila taarifa kutoka Bukoba na ofisi ya Ofisa Utamaduni Muleba zinasema siyo kweli…” ameandika Meena.
Kuhusiana na ajali ya boti, Meena amesema, “…ni kweli kwamba kuna boti imezama katika Ziwa Victoria, na kulikuwa na uvumi mwingi mjini Bukoba na Wilayani Muleba kuhusu mwanamuziki huyo kufariki lakini baadaye ikathibitika kwamba hakuwa mmoja wa abiria.”
Nayo Upland FM radio, Kwa kupitia Facebook page yake, imekanusha taarifa za kufariki Saida karoli na kusema msanii huyo ni mzima wa Afya. “TAARIFA: Kumezuka habari zisizo rasmi juu ya mwanamuziki SAIDA KALORI. Tunaomba kuthibitisha kwa Mwanamuziku huyo ni MZIMA wa afya kabisa. Usidanganywe na uzushi wowote. ASANTE.” imesema taarifa hiyo ya Upland FM

chanzo:BlogSy Tanzania http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: