UNANAFASI? SOMA HAPA" MADAWA YA KULEVYA TISHIO KWA VIJANA

...................

yamezima ndoto za wengi ambapo wengine wamekatisha hata uhai wao

Mabondia wa Tanzania wafungwa Mauritius


Mabondia waliohukumiwa

Mabondia wanne wa Tanzania wafungwa miaka 15 jela nchini Mauritius kwa makosa ya kuingiza dawa za kulevya aina ya heroin.

Mabondia hao ni Case Ramadhani Fills, Nathanael Elia Charles, Ally Rajabu Msengwa na Petro Charles Mtagwa.
Wakati kesi hiyo ilipoanza kusikilizwa, wote walikiri makosa ya kuingiza mihadarati hiyo nchini Mauritius wakati walipokwenda kushiriki mashindano ya ndondi barani Afrika mwaka 2008.
Wakiwa mbele ya Jaji, waliiambia mahakama kuwa walilazimika kuingia katika biashara hiyo haramu kutokana na hali zao za maisha kuwa maskini.
"Tunaomba radhi kwa taifa la Mauritius", waliiambia mahakama.
"Tu watu maskini na tunategemewa na familia, watoto na wazee wetu wanaotugemea."
"Kwa dawa hizi tungepata kiasi cha Pauni £4,000". walisema
Jaji Benjamin Marie Joseph alisema katika kutoa adhabu hiyo yote hayo ameyafikiria, kwani walitoa ushirikiano mzuri wakati wote wa uchunguzi wa kesi hiyo, kulikowezesha hata wafanyabiashara hiyo, raia wa Mauritius kukamatwa.
Wamekuwa mahabusu kwa siku 1,722, sawa na miaka miatano, hivyo watatumikia miaka kumi iliyobakia jela. Pia watatakiwa kulipa faini ya pauni £1,600 na gharama nyingine za uendeshaji wa kesi hiyo.
Kwa mujibu wa mwandishi wa habari wa BBC nchini Mauritius Yasine Mohabuth in Mauritius, Jaji aliwashutumu kwa kuukosea umma wa Mauritius kwa kuingiza dawa hizo za kulevya aina ya heroin.
Mabondia hao waliwasili Mauritius tarehe 10 Juni 2008 na kuweza kupita uwanja wa ndege bila kunaswa hadi walipokamatwa katika hoteli waliyofikia ya Quatre Bornes.
Kwa pamoja walimeza gram 4639.04 za heroin zikiwa katika vifuko 358 vijulikavyo kama pipi.


Dawa za Kulevya TZ - Vijana waathirika

Dawa za kulevya Tanzania

Dawa za kulevya ni kosa la jinai katika nchi nyingi duniani. Lakini matumizi ya dawa hizo, hususan miongoni mwa vijana nchini Tanzania, umekita mizizi kwa sababu dawa za kulevya kama vile bangi hupatikana kwa urahisi nchini humo.
Ngwandume Joseph, alielezea BBC kuwa alianza kuvuta bangi tangu utotoni, tabia iliyomuingiza mashakani.

" Mimi nilianza kuvuta bangi nikiwa darasa la sita. Nilijiunga na vijana waliokuja shuleni kucheza mpira na nikadhani kuwa ni ujasiri kujiingiza katika matumizi hayo". Asema Ngwandume. Lakini aligundua kuwa sio sifa bali anajijutia." kutokana na tabia mbaya niliyoshika, nilifukuzwa shule licha ya kuwa nilikuwa nimefuzu vizuri. Sasa najuta"

Serikali inasemaje?

Tume inayodhibiti dawa za kulevya inakiri kwamba mtandao wa wafanyibiashara vigogo unachangia kurudisha nyuma vita dhidi ya dawa za kulevya. Kamishna mkuu wa tume hiyo nchini Tanznia ni Christopher Shakiondo. " Bangi kwa mfano inalimwa katika sehemu nyingi na inapatikana kwa urahisi sana. Wengine wanalima hata nyuma ya nyumba zao na hivyo watoto pia wanaweza kupata".
Sasa vijana walioathirika na dawa kama hizo wamepiga moyo konde na kuamua kuanza maisha upya kwa matumaini.
Ngwandume alieleza BBC siri yake." Tulipata elimu muhimu shuleni kuwa tuangalie 3Ts. Tatizo - Tatuzi na Tokeo. Ukifikiria hizi basi utajua ni wapi unelekea au ni nini kitakachotokea hapo mbeleni - na utaweza kujiamulia hatma yako".


Masoko ya Mihadarati yaanguka

Dawa aina ya Cocaine
Masoko ya Mihadarati yanaanguka
Shirika la umoja wa mataifa linalohusika na dawa za kulevya na uhalifu UNODC, linasema kuwa masoko ya dunia kwa mihadarati kama Cocaine, Opium na bangi yanaendelea kuanguka.
Lakini katika ripoti yake ya kila mwaka shirika la UNODC limesema uzalishaji wa madawa yasio asilia kunazidi kuongezeka.
Ripoti hiyo kuhusu matumizi ya dawa za kulevya duniani inasema ukulima wa kasumba katika Afghanistan,ambako hukuzwa asilimia 74 ya kasumba duniani kulipungua kwa kiwango cha asilimia 38 mwaka jana , kwa sababu ya maradhi yaliyoangamiza sehemu kubwa ya zao la maua yanayozalisha kasumba.
Lakini shirika hilo la umoja wa mataifa la kupambana na uhalifu na dawa za kulevya UNODC limeonya kwamba haielekei kwa hali hii ya kupungua uzalishaji kasumba utaendelea.
Ripoti inasema ulimaji wa zao la opium katika Burma uliongezeka kwa asilimia 20 mwaka jana.
Na ilionya kuwa kusini Mashariki mwa Asia imegeuka kuwa kituo kikuu kwa sababu ya kuongezeka sana kwa dawa zisizo asilia.
Ilisema matumizi mabaya ya dawa za matibabu ni tatizo linalozidi kukua.
Ripoti hiyo inasema utengenezaji wa Cocaine ulipungua lakini bado kuna matumizi makubwa ya mhadarati huo katika Marekani na Ulaya.


Kasumba inapitia Afrika Mashariki

Ripoti ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa wanaofanya magendo ya mihadarati Afrika sasa wanapitia Afrika Mashariki,
kwa sababu ya vikwazo vingi Asia na Mashariki ya Kati, na hivo kuleta uvunjaji wa sheria na matumizi zaidi ya mihadarati katika eneo hilo la Afrika Mashariki.
Wanajeshi wanapita shamba la kasumba, Helmand, Afghanistan
Inakisiwa kuwa biashara ya mihadarati ilifika dola bilioni 68 dunia nzima, katika mwaka wa 2009.

Ofisi ya Kupambana na Mihadarati na Uhalifu ya Umoja wa Mataifa, inasema ina wasiwasi kuwa Afrika Mashariki imekuwa njia inayotumiwa na wafanya magendo, kwa sababu kanda hiyo haina uwezo wa kupambana na magendo na uraibu wa mihadarati.
Inasema madawa ya kulevya na idadi ya walanguzi waliokamatwa, inaonesha kuwa wafanya magendo hayo, hasa magengi kutoka Afrika Magharibi, wanazidi kusafirisha kasumba kutoka Afghanistan na Pakistan kupitia Afrika Mashariki, kisha kupeleka Ulaya na kwengineko.
Afghanistan ndio mzalishaji mkubwa kabisa wa kasumba, na asilimia 40 hupitishwa Pakistan, kabla ya kuelekezwa kwengineko.
Ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa inasema katika miezi mitatu ya mwanzo ya mwaka huu, shehena mbili za kasumba, kila moja zaidi ya kilo mia moja, zimeripotiwa Kenya na Tanzania.
Inaeleza kuwa sababu ya magendo hayo kuzidi ni rushwa, umaskini na uwezo haba wa idara za kuweka sheria.

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: