Madaktari wa Mandela wabadili msimamo wa kuzima mashine

...................

Kwa ufupi
Madaktari hao, wameishauri familia hiyo kuachana na ushauri wa awali wa kuindoa mashine hiyo, hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili kitakaposhindwa kufanya kazi.


Johannesburg. Madaktari wanaomtibu Rais wa zamani wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, wamebadili msimamo wao wa awali wa kuiondoa mashine inayomsaidia kupumua kiongozi huyo, kwa maelezo kuwa hali yake si mahututi.
Madaktari hao, wameishauri familia hiyo kuachana na ushauri wa awali wa kuindoa mashine hiyo, hadi tu pale moja ya kiungo chake muhimu cha mwili kitakaposhindwa kufanya kazi.
Mmoja wa marafiki wa karibu na mpigania uhuru ambaye aliwahi kufungwa pamoja na Mandela, Denis Goldberg, amesema madaktari hao waligusia kuhusu suala la kuondoa mashine lakini baadaye walikataa kwa kuwa Rais huyo hayuko katika hali mbaya kiasi cha kukata tamaa.
Goldberg alieleza kuwa Mandela ana uwezo wa kupata nafuu, kwani anaweza kusogeza baadhi ya viungo na kutambua sauti.
Juzi vyombo vya habari vya hapa nchini vilitoa hati ya kiapo ya Mahakama, ikionyesha kuwa madaktari hao waliishauri familia ya Mandela kuondoa mashine ya kumsaidia kupumua kwani, ‘asingeweza kuendelea kuishi’.
Sintofahamu
Taarifa hizi zimekuja wakati ambapo wanafamilia ya Mandela ambao walikwenda mahakamani kwa ajili ya kesi ya kufukua miili ya watoto watatu wa Mandela kuandika katika ripoti ya Mahakama kuwa Rais huyo alikuwa mahututi.
“Ni kweli kuwa hali ya Mandela ni mbaya, lakini si kama ambavyo baadhi ya vyombo vya habari vimekuwa vikiandika” alisema Goldberg.
Ushuhuda wa mwisho uliotolewa na wanafamilia hiyo mahakamani, umedaiwa kuwa ulikuwa ni mbinu tu ya kuharakisha hukumu dhidi ya mjukuu wa Mandela, Mandla.
Kauli ya kuwa hali ya Mandela ilitiwa chumvi ili kuharakisha hukumu ya Mahakama, imetolewa wakati Ofisi ya Rais ya Afrika Kusini ilipoitaka familia hiyo kutatua mgogoro wa maziko.
“Inasikitisha kuwa kuna mgogoro katika familia hiyo na tungependa utatuliwe mapema iwezekanavyo” alisema msemaji wa Rais Jacob Zuma, Mac Maharaj jana.
Hata hivyo, Maharaj alikataa kuzungumzia kuhusu hati ya Mahakama ambayo ilieleza kuwa Rais huyo wa zamani mwenye miaka 94, yupo mahututi na kuwa madaktari wameshawashauri wanandugu kuondoa mashine ya kupumulia.

chanzo:unapitwa.com
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: