TOP 10 YA WASANII MATAJIRI BARANI AFRIKA.

...................



 (1). Youssou N’dour – Senegal
 Youssou N’dour ni msanii nguli na maarufu kutoka nchini Senegal na Africa kwa ujumla, staili anayotumia kuimba mwanamuziki huyu inafahamika kama Mbalax ambao ni mchanganyiko wa lugha za asili nchini Senegal ikijumuisha Rumba, Jazi, rock pamoja na soul, kazi yake muziki imeweza kufanya aweze kumiliki mojawapo ya majengo makubwa ya media nchini Senegal chenye kituo cha Radio pamoja Televisheni ndani yake pia alipata nafasi ya kuchaguliwa kuwa waziri wa Utalii na utamaduni mwaka 2012 pia alipata dili la kurekodi wimbo wa ”La Cour des Grand” ambao ulitumika kama National Anthem katika fainali za kombe la Dunia mnamo mwaka 1998 akishirikiana na mwanamuziki mwenzake Axelle Red.
(2). P Square – Nigeria
Hakuna asiyewafahamu Mapacha hawa Peter na Paul Okoye  wanaotamba na ngoma yao ya ”Personally” ambao wanatokea nchini Nigeria, Mapacha hawa wanaosifika kwa kutoa shoo kali na kabambe kazi yao ya muziki imewawezesha   kupata tuzo kubwa mbalimbali ikiwemo ile ya KORA AWARDS mwaka 2010 wakitajwa  kama wasanii bora wa mwaka na kwa sasa kiasi wanachoingiza kwa shoo moja ni dola za kimarekani 150,000 wakiwa na mjengo mmoja nchini Marekani uliowagharimu zaidi ya Dola Milioni 3 za kimarekani hiyo inawafanya washike nafasi ya pili.
(3).D’banji – Nigeria
Dapo Daniel Oyebanjo Maarufu kwa jina la steji D’BANJI au unaweza ukamwita KOKO MASTER kutoka nchini Nigeria ambaye  alianza kusikika rasmi kwenye miaka ya 2007 alipotoka na kibao cha Fallin In Love kilichobamba kwa kipindi kirefu katika vituo mbalimbali vya media huku akimshirikisha mwanama ‘Geneviv Nnaji’ ambaye ni muigizaji nyota wa filamu Nigeria katika video ya wimbo wake huo, D’BANJI ndiye mwanamuziki wa kwanza kutoka barani Africa kujiunga katika rekodi kubwa ya muziki duniani ya GOOD MUSIC inayomilikiwa na Rapa Kanye West huku akiwa amechukua tuzo za kutosha kupitia kazi yake ya sanaa, Baadhi ya vitega uchumi alivyonavyo mwanamuziki huyo kupitia muziki ni pamoja na Klabu ya usiku anayomiliki iliyopo nchini Nigeria, Brand yake ya maji inayofahamika kwa jina la KOKO WATER na Reality Show yake ya KOKO MANSION pia ni kati ya wasanii wanaoingiza mpunga mrefu katika shoo zao.
(4).Koffi Olomide – DR Congo
(5).Salif Keita – Mali
(6).Fally Ipupa – DR Congo
(7). 2 Face Idibia – Nigeria
(8). Hugh Masekela – South Africa
(9). Banky W  –  Nigeria.
(10). Jose Chameleone – Uganda( East Africa).


Na larrybway
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: