Majanga:Benki za Ugiriki kufungwa.

...................

Waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras amesema Jumapili kuwa benki za nchi hiyo huenda zitafungwa na utoaji wa fedha taslimu ukawekewa masharti.
Waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras katika picha ya awali.
Waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras katika picha ya awali.

Waziri mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras amesema Jumapili kuwa benki za nchi hiyo huenda zitafungwa na utoaji wa fedha taslimu utawekewa masharti kutokana na mzozo kuhusu deni kati ya Athens na wakopeshaji wa kimataifa kutopata suluhisho. Katika taarifa aliyoitoa kwenye televisheni ya taifa, Bw Tsipras amelaumu wakopeshaji kwa mzozo huo ambao unatishia Ugiriki kuondolewa kwenye uanachama wa mataifa 19 yanayotumia sarafu ya Euro. Hata hivyo hakubainisha ni muda gani ambao benki  za Ugiriki zitafungwa  wala athari za udhibiti wa mitaji. Muda wa kupatiwa msaada wa kifedha  unakwisha Jumanne wakati Ugiriki inataka isaidiwe dola bilioni 8 zaidi ili iweze kulipa deni la dola bilioni 1.8 kwa shirika la kimataifa la fedha  IMF. Lakini Athens inasita kutekeleza masharti   yaliyotolewa na  wakopeshaji  ya kubana matumizi ikiwa ni pamoja na makato zaidi ya  malipo ya uzeeni. Benki kuu ya Ulaya imesema kuwa imeweka fedha za dharura kwa benki za Ugiriki wazi wakati kukiwa na misururu mirefu  kwenye mashini za kutolea pesa, watu wakijaribu kutoa fedha walizoweka kwenye mabenki.

chanzo:VOA
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: