Rais wa Misri asaini sheria kali dhidi ya ugaidi.

...................

Rais wa Misri Abdel-Fattah el-Sissi akizungumza na wananchi kwenye msiba wa mwendesha mashitaka mkuu wa Misri Hisham Barakat, akiwa na wanafamilia wake.
Rais wa Misri Abdel-Fattah el-Sissi akizungumza na wananchi kwenye msiba wa mwendesha mashitaka mkuu wa Misri Hisham Barakat, akiwa na wanafamilia wake.
Rais wa Misri Abdelk Fatah El Sisi amesaini sheria mpya ya kupambana na ugaidi jana Jumapili ambayo inatoa hukumu ya kifo na kifungo cha maisha jela  kwa baadhi ya makosa na pia kutishia faini kubwa kwa ripoti za uongo juu  ya mashambulizi ya kigaidi.
Bw.Sisi aliahidi mwezi Juni  kuweka sheria kali za kupambana na ugaidi   baada ya mwendesha mashitaka mkuu wa Misri  kuuwawa kwa bomu . Makundi mawili ya wanamgambo   yalidai kuhusika na shambulizi. Lakini rais huyo amelishutumu kundi la Muslim Brotherhood ambalo serikali yake imelitaja ni  taasisi ya  kigaidi na kulikandamiza  tangu alipoongoza kuondolewa  mamlakani kwa rais mwenye msimamo wa serikali ya kiislam Mohamed Morsi Julai 2013.
Chini ya sheria mpya wale wanaoongoza au kuanzisha makundi ya kigaidi huenda wakakabiliwa na adhabu ya kifo. Kufadhili ugaidi  kunaweza kupelekea adhabu ya  kifungo cha maisha wakati kuchochea kitendo cha kigaidi au kujiandaa kuchochea shambulizi kunapelekea kifungo jela

chanzo:VOA
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: