Upinzani Uingereza wana kiongozi mpya

...................


Jeremy Corbyn
Chama kikuu cha upinzani cha Uingereza cha Labour kimemchagua kiongozi mpya, Jeremy Corbyn, wa siasa za mrengo wa kushoito.
Alishinda kwa kishindo ingawa alipoanza hakufikiriwa kabisa kuwa atafikia uongozi.
Corbyn ameongoza katika kampeni akiwa na ajenda ya mabadiliko makubwa, pamoja na azma ya kutaifisha tena sekta fulani za uchumi.
Mapendekezo yake yamepokewa vema na wale waliochoka na sera za kubana matumizi, na kile wanachoona kuwa wanasiasa wakuu wasiofahamu hali ya mtu wa kawaida.
Wagombea wengine watatu walitaka chama cha Labour kibaki katika siasa za wastani.
Katika hotuba yake baada ya kuchaguliwa, Bwana Corbyn alilaani kile alichosema ni tofauti ya kuchusha baina ya matajiri na mskini.
Alisema nchama chake kina umoja na kimeazimia kuleta jamii inayoheshimika na njema zaidi.

chanzo: http://www.bbc.com/swahili/habari/2015/09/150912_new_labour_leader
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: