Polisi ajipata 'danguroni' kimakosa

...................


 
 Konstabo wa polisi Mike Ober alidhaniwa kuwa mwanamume wa kukodiwa kuwatumbuiza wanawake 
 
Tembea tembea ya afisa mmoja wa polisi nchini Uingereza nusura imtumbukize ''pabaya'' alipoingia katika jumba moja la starehe lililokuwa limekodishwa kwa minajili ya kuandaa sherehe ya wanawake kuadhimisha miaka 50 ya mwenyeji wao.
Konstabo wa polisi Mike Ober alikuwa katika pita pita yake katika eneo la Avon Uingereza aliposhangaa kuona mlango klabu moja maarufu ikiwa wazi.
Aliposogelea kupeleleza kunani , alipigwa na butwaa, wanawake walipomshangilia kwa ''huba'' na ''uchu''.
Wengine walimtaka avue nguo mara moja ili ''awatumbuize''
Aliulizwa kama ndiye aliyeagizwa awape burudani ?
Ndipo akang'amua kuwa siye aliyekuwa anatarajiwa ila ni mwanaume wa kukodiwa kuwatumbuiza mabibi waliokuwa wanasheherekea miaka 50 ya mmoja wao ,,,''alilazimika kuondoka mara moja.''
''Mbona umekuja mapema sana?''
''Tupe muda kidogo tujiandae kidogo kisha urejee'' alimweleza bi kizee mmoja.
''Nililazimika kuondoka mara moja'' alisema afande huyo mwenye umri kati ya miaka 20-27.
Alipokuwa akiondoka alikutana na mwanamume mmoja akifululiza kuelekea ndani ya jumba hilo la starehe

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: