KWANINI TANZANIA TU KILA SIKU....?

...................


.
Tuna maswali mengi ya kujiuliza kwanini Timu yetu ya Taifa haifanyi vizuri katika mashindano mbalimbali. Tukijiuliza tunapata majibu mengi sana ya kweli na yakufikirika.

KUHUSU MECHI NA WAZIMBABWE NINA YANGU YA KUSEMA
Kwanza kabisa poleni Watanzania kwa kuendelea kuumizwa na matokeo. Lakini safari hii natoa lawama kwa Uongozi wa mpira nikimaanisha TFF. Walichokifanya ni kutimiza wajibu na sio kufanya sehemu ya majukumu yao ya kikazi ya kuwatumikia watanzania na kuhakikisha tunapata ushindi.
Ni jambo la kushangaza uongozi wa mpira Tanzania kushindwa kuweka ratiba inayoelewka ya Timu ya Taifa.  Ikumbukwe kuwa FIFA hutoa ratiba yao mapema na ndipo Mataifa mengi hupanga ratiba kwa kuzingatia kalenda ya FIFA. Ligi zote duniani zilisimama kuweza kuipa nafasi FIFA itemize ratiba yake kwa timu za kufuzu kombe la dunia na mechi za kirafiki.

Swali la kujiuliza
Kulikuwa na umuhimu gani wa TAnzaia kumaliza mzunguko wa ligi katikati ya wiki wakati tuna mechi ya kirafiki weekend?

Kwa hili wachezaji hawajapumzika wala hawaja kaa kambini kuweza kutengeneza good chemistry kwaajili ya mechi na wazimbabwe. Kulikuwa na haja gani kumaliza mzunuko , kasha kucheza mechi ya kimataifa na kupumzika kwa maana ya mapumziko baada ya mzunguko wa kwanza? Kwanini tusinge ipa timu ya Taifa muda wa wiki mbili kasha ligi yetu tukamalizia weekend ijayo kasha tupumzike? Au zengwe kwa kocha aonekane ameboronga kasha tumtimue?
Kwa upande mwingine Tanzania mpira sio fani yetu ama viongozi wa mpira wapo kwaajili ya kuionyesha dunia kuwa na sisi tunashiriki mpira wa miguu.

Kama kweli Tunataka kupata maendeleo ya mpira basi tujifunze zaidi ama tulete mkoloni atutawale tena kwenye mpira tu pengine tutapata mwelekeo lakini kwa tulipo sasa hali ni tete
 


http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: