UNATAKA UFADHILI WA MASOMO AU MTAJI WA BIASHARA

...................

ufadhili wa masomo
Kama wewe ni mmoja wa wanaotafuta ufadhili wa masomo au msaada wa kifedha ili ujiendeleze kielimu au kibiashara , basi makala hii inakuhusu sana.

Katika makala ya MAMBO 4 YA MSINGI ILI KUPATA SCHOLARSHIP YA ELIMU

nilitaja mambo ya kuzingatia ili kupata schorlaship. Hata hivyo kuna jambo moja nimeliona likijirudia mara kwa mara na ambalo sikulitaja katika makala ile. Nakushauri ukaisome ile makala yote vizuri pia. BOFYA HAPA KUSOMA HAYO MAMBO 4
Kupata ufadhili wa masomo kunaanzia katika kujiweka katika mazingira ya kuanzisha na kuendeleza mawasiliano na watu maalum ambao wanaweza kukupatia huo ufadhili wa masomo au mtaji wa biashara.
Kuna namna nyingi ya kuwapata watu wanamna hiyo. Katika makala nyingine tutajadili jinsi ya kujijengea mazingira ya kukutana na watu wanaoweza kuwa wafadhili wako. Leo tujifunze jambo la msingi zaidi ili hata ukikutana nao uweze kuwakamata kuwa wafadhili wako.
Katika makala hii nataka nikusisitize swala hili la msingi la Kuweza Kufanya Mawasiliano Fasaha. Jambo hili ni dogo ila ukilipatia vizuri litakujengea fursa kubwa hata kama una mapungufu katika baadhi ya maeneo.
Ninaposema kufanya mawasiliano  fasaha namaanisha yafuatayo:

Tafuta kujisikia kuvutiwa na mtu unayewasiliana nae:
Watu hufanya mawasiliano na watu ambao wanaonekana kutaka kufanya mawasiliano. Penda kumuachia nafasi mtu unayewasiliana nae ili akupashe yaliyo yake. Onyesha kutaka kufahamu zaidi kwa kuuliza maswali na kukumbuka anayokuambia. Onyesha kuwa unajali na kuwa upo tayari kusikiliza zaidi na zaidi.

Kuwa mwenye kujua vitu vingi:
Wewe pia unahitaji kuwa mwenye mazungumzo yanayovutia. Uwe na uwezo wa kuchanganya mazungumzo ya namna nyingi kutegemea na aina ya mtu unayewasiliana nae iwe ni mambo ya kiimani, siasa, burudani, habari za kitaifa, kimataifa, michezo, vichekesho na hata ya fani husika.

Jua anayojua au kupendelea mtu unayewasiliana nae:
Mara nyingi katika mawasiliano tunajikuta tuna shauku ya kujielezea sisi wenyewe, mambo yetu na jinsi tulivyo bora kiasi cha kupoteza nafasi ya kusikia na kujifunza nini mtu mwingine anajua , anafuatilia na kupendelea. Mfano ukijua vitu anavyopendelea na yapi anafahamu au anajifunza mtu unayewasiliana nae, ni rahisi nawe kujifunza hayo mambo au kufuatilia ili uwe na yapi katika kuendeleza mawasiliano yaliyo na mvuto kwa mtu husika.
Kwa namna gani hii itakusaidia ?
Uwezo wako wa kuwasiliana kwa ufasaha na kuendeleza mawasiliano kutamfanya mhusika unayetaka akupe ufadhili wa masomo au mtaji akufahamu vizuri na avutiwe nawe. Na ni rahisi mtu kutoa ufadhili kwa mtu anayempenda na kumjali. Hivyo kwa kutengeneza mawasiliano bora unajifanya “promo” kuwa wewe unafaa kusaidiwa. Na ni promo ya ukweli kwani mfadhili anapata kukufahamu vya kutosha na yeye mwenyewe kujikomit kukusaidia.

Hitimisho: 
Katika mazungumzo yako usiweke mbele kutangaza shida zako au kuomba msaada wa ufadhili wa elimu au mtaji wa biashara. Fanya mazungumzo kwanza, jenga mahusiano. Muache muhusika mwenyewe ajisikie hitaji la kukusaidia. Na kama mhusika ana uwezo kweli, na mmejenga uhusiano mzuri, wala usihofu, kwani marafiki husaidiana. Atakusaidia tuu.
 
 
chanzo: http://mbuke.blogspot.com.co
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: