Safari ya kupata elimu:kwa Tanzania ni kazi kwelikweli(noma)
Sylvia ni msichana wa miaka
minane anaishi kijiji kimoja Tanzania, licha ya maisha yake amejitolea
kupata elimu na kila siku hutembea kwa saa moja unusu kwenda shuleni.
Yeye ni miongoni mwa wasichana waliobahatika kupata elimu Barani Afrika
Mtoto huyu hupitia njia nyingi
familia yake ni masikini na haiwezi kumnunulia viatu. Japo hakuna karo
anayolipiwa, imekua vigumu kwa wazazi wake kununua vitabu au sare za
Sylvia za shule.
Safari ya msichana huyu kisha
inampeleka barabara kuu. Wakati mwingine kuna jua kali, vumbi nyingi.
Msimu wa jua barabara hujaa mapote na inampa changamoto msichana huyu
katika safari yake shuleni
Ikiwa msichana huyu hataki vumbi
na matope ya barabara, huamua kupitia kwenye njia ya reli. Hata hivyo
kuna hatari zake, treni huenda ikaamkanyanga. Wakati mwingine watoto wa
shule wamekua wakitekwa nyara.
Kuna vichochoro vingine kando ya
barabara kuu ambavyo Sylvia hutumia, lakini kuna hatari ya kukumbana na
wabakaji.
Baada ya pita pita hizo hatimae
Sylvia huwasili shuleni.Msichana huyu anasema ataendelea na elimu yake
licha ya safari ndefu ambayo hufanya kila siku.
Kwa mujibu wa shirika la Umoja wa
Mataifa la elimu na Utawaduni-UNESCO asili mia 62 ya wasichana Afrika
wameweza kuingia shule za upili, hata hivyo nchini Tanzania ni asili mia
32 pekee ya wasichana ambao wanaweza kujiunga na shule za upili.
11 Julai, 2013 - Saa 10:34 GMT
11 Julai, 2013 - Saa 10:34 GMT
Baba wa kambo wa Sylvia amekua
akiona malezi yake kama mzigo hasa elimu, lakini kwake Sylvia anasema
elimu ni njia pekee ya kubadilisha maisha ya familia yake
chanzo:bbcswahili.
chanzo:bbcswahili.
0 comments: