MGOMO MKUBWA: Chama cha walimu kuitisha mgomo wa walimu usio na kikomo

...................

Chama cha walimu wilaya ya MISENYI mkoani Kagera wanatarajia kuitisha mgomo usiokuwa na kikomo kwa kutofundisha katika shule za msingi na sekondari endapo uongozi wa halmashauri ya wilaya ya misenyi wataendelea kupoteza nyaraka zao mbalimbali zikiwemo
Za madai ya malipo na zile za kupandishwa madaraja.

Kwa mujibu wa taarifa lilyorushwa na ITV ni kwamba baada ya uchaguzi wa viongozi wa chama cha walimu wilaya ya misenyi wamesema kuwa katika kikao cha utekelezaji CWT imeutaka uongozi wa halmashauri ya wilaya ya misenyi kutatua migogoro ya waimu katika kipindi cha wiki mbili na watakapokaidi chama cha walimu kitaitishwa mgomo kwa walimu wote wa shule za msingi na sekondari bila kujali kuwa wakati huu ni wakati wa kuandaa wanafunzi kufanya mitihani ya taifa.
Akijibu malalamiko hayo kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Misenyi Bw. Moses Gwaza amekanusha vikali tuhuma hizo na kusema kuwa katika kipindi cha miezi mitatu serikali imelipa madeni ya walimu katika wilaya ya Misenyi zaidi ya shilingi miioni 338 na kwamba walimu 96 madai yao hayapo kwenye bajeti ya mwaka huu na kuwataka kuwa na subira wakati serikali ikijipanga kuwalipa.
Halimashauri kuu ya CCM wilaya ya ikungi imemuagiza mkuu wa wilaya hiyo kufuatilia matumizi mabaya ya shilingi zaidi ya milioni mianne za mfuko wa jimbo la singida mashariki,jambo ambalo limesababisha miradi mingi ya maendeleo kushindwa kukamilika.
Akitoa maadhimio hayo katibu wa CCM wilaya ya ikungi Bwana. Aluu Segamba amesema baada ya  kukagua utekelezaji wa ilani ya CCM katika wilaya zote  walibaini jimbo la  singida mashariki lina matumizi mabaya ya mfuko wa jimbo ,huku fedha hizo ni za serekali na zinatakiwa kuwanufaisha wananchi wote bila kujali  vyama vya siasa.
Katika hatua nyingine Bwana. Segamba amewaomba baadhi ya viongozi wa dini wenye tabia ya kuingilia maswala ya siasa waache  kuongoza dini zao na waingie kwenye ulingo wa siasa,pia ameiomba serekali wilayani ikungi kukaa na viongozi hao  iliwakawaeleze waumini wao  kujitokeza kujiandikisha katika daftari la kudumu  la kupiga kura na kuacha kuwashawishi waumini kupigia kura  katiba  ndiyo au hapana,kwa kufanya hivyo inaweza kusababisha uvunjifu wa amani.
kwa upande wake mkuu mpya wa wilaya ya ikungi,Gishuli Charles,ameahidi kuzifanyia kazi tuhuma hizo zilizotolewa na CCM,ili kujijengea mazingira mazuri ya kuchukua hatua za kisheria endapo atajiridhisha na tuhuma hizo.
thanks:eddy blog
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: