PADRE AACHA KANISA NA KUUFUATA UBUNGE MBOZI, SABABU ZA KUFUATA UBUNGE HIZI HAPA,,,!
Padre wa kanisa la Angikana Jonathan Mwashilindi akikabidhi Bendera ya Chama kwa viongozi wa Chadema kata ya Nanyala kama njia ya kukijenga chama hicho.
HABARI KAMILI
Padre wa kanisa la Angikana Jonathan Mwashilindi amesema amechukua uamuzi wa kugombea Ubunge katika jimbo la Mbozi Mashariki ili aweze kupata fursa ya kutumikia makundi mengi ya kijamii zaidi ya kanisani.
Mwashilindi
ameyasema hayo katika maeneo na nyakati tofauti alipozungumza na makada wa
Chama cha Demokrasia na Maendele(Chadema) kwenye kata mbalimbali za wilayni
Mbozi alizotembelea zikiwamo za Nanyala,Ipunga na Miyovizi.
Akizungumzia
nia yake ya kugombea kwa makada wa chama hicho,Pade Mwashilindi amesema kwa miaka 13
aliyolitumikia kanisa la Anglikana amekuwa akihudumia jamii ya aina moja na
sasa ameona ni wakati kwake kutanua wigo wa kuitumikia jamii kwa kuingia kwenye
siasa badala ya kanisani.
Padre
huyo mzaliwa wa kijiji cha Mpanda wilayani Mbozi,amesema wakazi wilayani humo
bado wanakabiliwa na changamoto nyingi hali inayotokana na viongozi wa
kuchaguliwa kutowajibika ipasavyo.
Moja
ya changamoto alizozitaja kuwakabili wakazi wa Mbozi ni pamoja na kutonufaika
na shughuli za kilimo ambazo kwa miaka mingi wamekuwa wakijishughulisha nazo na
kuzitegemea kama chanzo kikubwa cha pato lao.
chanzo:lyamba la mfipa

0 comments: