CCM YAPATA PIGO,MGOMBEA WAKE WA UDIWANI AFARIKI DUNIA GHAFLA.

...................



Chama cha Mapinduzi Jimbo la Mbeya Mjini kimepata pigo baada ya mgombea wake wa Kata ya Uyole, Kambi Njela , pichani juu) kufariki dunia ghafla. 

Njela ambaye alianza kampeni mwezi uliopita aliugua ghafla akiwa anaendelea na kampeni zake na kwamba dalili za ugonjwa zilianza kwenye miguu ambayo ilionekana kupata ubaridi na hatimaye homa kali. 

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mbeya, Ephrahimu Mwaitenda amesema kifo hicho ni pigo kubwa kwa chama hicho kwani marehemu alipita bila kupingwa kwenye kura za maoni, hivyo tayari walikuwa na ushindi mkononi 

Naye meneja wa Kampeni za CCM Wilaya ya Mbeya mjini,Charles Mwakipesile amesema kuwa marehemu alikuwa mchapa kazi na aliweza kuisimamia vizuri Ilani ya chama chake katika kata yake na ndiyo ilikuwa inaongoza kwa maendeleo. 

“Alifanya vizuri kwenye kata yake na ndiyo maana hakuweza kupata upinzani na hatimaye kupita bila kupingwa hivyo tumempoteza mtu muhimu sana ndani ya chama na tumeipoteza kata hiyo ambayo tayari ilikuwa mikononi mwetu”amesema Mwakipesile 

Kwa upande wake Msimamizi wa uchaguzi Jimbo la Mbeya, Musa Zunguza amesema kutokana na kifo hicho taratibu zinafanyika kusimamisha kampeni za udiwani kwenye kata hiyo
 
chanzo:magicnewstz.blogspot.com
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: