KORTINI KWA KUMTUKANA MKE WA RAIS

...................

Mbunge ashtakiwa kumtusi mke wa Mugabe

Mugabe 
Bi Mugabe huitwa mama na wafuasi wa chama cha Zanu-PF
 
Mbunge mmoja wa chama tawala nchini Zimbabwe anatarajiwa kufikishwa kortini kujibu mashtaka ya kumtusi mke wa Rais Robert Mugabe, Grace Mugabe.
Mbunge huyo Bw Justice Wadyajena anadaiwa kutumia “lugha ya matusi” dhidi ya mwanachama mwenzake wa chama tawala cha Zanu-PF aliyekuwa ameweka picha ya Bi Mugabe kwenye gari lake.
Kisa hicho kinatazamwa na wengi kama sehemu ya vizozo ya ndani ya chama kuhusu nani atamrithi Rais Robert Mugabe ambaye atatimiza umri wa miaka wa miaka 92 Februari.
Bw Wadyajena amenukuliwa kwenye nyaraka za mahakama kwamba alimwambia Jimayi Muduvuri: "Wewe ni mjinga sana, sawa na mama huyu wenu.” Atafikishwa kortini Victoria Falls.
Mke wa rais nchini Zimbabwe huitwa "amai", maana yake mama, na wafuasi wa chama cha Zanu-PF.
Mbunge huyo amekanusha madai hayo.

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: