ZIFAHAMU NJIA 9 ZINAZOASHIRIA MWISHO WA DUNIA
Imeandaliwa na
MaendeleoVijijini Blog
WENGI wanapoambiwa kwamba mwisho wa dunia, yaani kiama,
utafika, mara nyingi hawaamini na wanaona ni kawaida kwa sababu watu wanazaliwa
wengine wanakufa.
Wapumbavu wamefikia hatua ya kukufuru wakisema kwamba mwisho
wa dunia ni pale unapokufa tu, siyo zaidi ya hapo huku wakisadiki tafiti za
kisayansi ambazo mara nyingi zinapingana na uwepo wa Mungu.
Wengine utawasikia wakisema; “Tangu enzi za mababu na mababu
tumeambiwa kuna mwisho wa dunia, Wakristo wanaamini Yesu atarudi, na waumini wa
dini nyingine nao wanaamini kuna kiama, lakini mbona hatuuoni huo mwisho wa
dunia?”
Hata hivyo, MaendeleoVijijini inaripoti bila shaka kuwa, zipo baadhi ya tafiti ambazo zimebainisha kwamba
mwisho wa dunia umekaribia.
Matukio ya sasa yanayotokea ulimwenguni, majanga, vita, mabaa
ya njaa, magonjwa ya ajabu na kadhalika ni dalili tosha kwamba mwisho wa dunia
umekaribia.
Tafiti mbali mbali za kisayansi nazo zinaashiria hivyo kama
ilivyoandikwa kwenye Vitabu Vitakatifu. Sayansi na teknolojia imeleta
mabadiliko makubwa ambapo hivi sasa dunia ipo kiganjani, wengine wanasema ni
kama kijiji tu.
Leo hii watu hawatembei na Biblia wala Qur’an, bali wanavipata
vitabu vyote kupitia kwenye simu zao za viganjani. Suala la kununua vitabu
linaonekana ni la kale sana, hakuna anayejisumbua kwenda kuuliza bei, achilia
mbali kununua. Hii inatokana na mafanikio makubwa ya tafiti za kisayansi na
kiteknolojia.
Lakini hebu jiulize, siku mitambo hiyo ya internet itakapozima
hali itakuwaje? Hiyo tafsiri yake ni rahisi sana, kwani itasadifu Maandiko
Matakatifu kwamba hata Neno la Mungu halitaonekana wala kupatikana tena. Si Biblia
wala Qur’an ambazo zitakuwepo kwa sababu hata mitambo ya kuchapa vitabu hivyo
hivi sasa inaweza kufungwa kutokana na kuingia hasara!
Hata hivyo, wanajiografia na mambo ya sayansi wameeleza mambo
yaliyodhahiri yanayotokea hivi sasa kama ni viashiria vya mwisho wa duniani,
hebu soka hapa:
Hollywood vs. Uhalisia
Majanga ya mabadiliko ya tabianchi na viumbe vya ajabu vyenye
sura za kutisha (aliens) ndivyo vitu ambavyo vimechukua sehemu kubwa ya filamu
za Hollywood vikiashiria mwisho wa mwanadamu katika sayari ya Dunia.
Kwa hakika, kuanzia filamu ya miaka ya 1950 ya "The Day
the Earth Stood Still" hadi filamu ya miaka ya 1960 ya "Planet of the
Apes" mpaka filamu za sasa kama "The Day After Tomorrow," na "After
Earth," kiama kimedhirika katika hadithi za kufikirika zinazoashiria
uhalisia.
Lakini najua kwamba, ingawa filamu hizi zinaweza kuwa za kufikirika na
kufurahisha tu, wanasayansi wengi wana hofu kubwa kutokana na matukio
yanayoendelea kutokea kila kukicha — mengine yakiwa mabaya kuliko hata yale
yanayoonekana kwenye filamu.
Kutoka kwenye magonjwa ya kutisha ya kuvu (fungus) hadi ujio
wa maroboti, kuna mabo tisa hapa ambayo wanasayansi wanayaona kwamba ni dhahiri
kuhusu mwisho wa dunia.
Kuongezeka kwa joto
duniani
Mabadiliko ya tabia nchi ndiyo mama wa hofu zote za mwisho wa
dunia, kwa sababu ndilo tishio kubwa linaloikabili dunia kwa sasa, kama
wanavyosema wanasayansi wenyewe.
MaendeleoVijijini
ambayo daima imekuwa ikiripoti habari za mazingira na maendeleo ya
uchumi kwa ujumla, hasa vijijini, inatambua kwamba mabadiliko ya
tabianchi yanaweza kufanya hali ya hewa yote
kuwa mbaya, yataongeza ukame katika maeneo kadhaa, kubadili mfumo wa
uzalishaji
wa wanyama pamoja na kuongeza magonjwa duniani, na kusababisha maeneo ya
dunia
yaliyo chini kuzama katika bahari ambayo inazidi kupanda juu.
Matokeo ya mabadiliko hayo yatasababisha machafuko ya kisiasa,
ukame wa kutisha, njaa, kuharibika kwa mfumo wa ikolojia na mabadiliko mengine
yatakayoifanya Dunia kuwa mahali pa kutisha na pasipofaa kuishi.
Vimondo!
Vimondo (Asteroids) ndivyo vinavyochukua sehemu kubwa katika
filamu za kutisha hasa zile za kisayansi, lakini wanasayanasi wanahofia kwamba
upo uwezekano pia wa jiwe kubwa kutoka angani, yaani kimondo, ambalo linaweza
kuporomoka na kuja kuikandamiza na kuifuta kabisa Dunia.
Inawezekana kimondo ndicho kilichowaua wale wanyama wakubwa wa
ajabu (dinosaurs) ambao tumeendelea kuwaona kama ni ngano za kufikirika na
kusadikika ingawa kweli walikuwepo ulimwenguni.
Na katika tukio la Tunguska, kimondo kikubwa kiliharibu eneo
la maili 770 (takriban kilometa 2,000) za msitu wa Siberia mnamo mwaka 1908.
Jambo linaloogofya, pengine, ni ukweli kwamba wanaanga
wanafahamu tu kuhusu kuporomoka kwa mawe ya angani ambayo yanaishia kwenye anga
za mbali katika mfumo wa jua (solar system).
Magonjwa ya kutisha
Majanga ya magonjwa mapya ya kutisha yanayoua bila tiba wala
kinga yanaibuka kila mwaka: Magonjwa yaliyoibuka katika miaka ya karibuni ni
pamoja na SARS (severe acute respiratory
syndrome), mafua ya ndege, na ugonjwa mpya kabisa wa MERS unaosababishwa na
virusi aina ya coronavirus ambao
ulianzisha Saudi Arabia. Hii ni mbali ya Ukimwi na Ebola. Na kwa sababu ya
maendeleo ya sasa yanayotufanya tuunganike bila shida, uchumi wa dunia, gonjwa
la kutisha linaweza kusambaa haraka kama moto wa nyikani.
MaendeleoVijijini
inazo kumbukumbu jinsi ugonjwa wa Ebola ulivyomaliza watu wengi hasa
Afrika Magharibi na bado unaendelea kuwa tishio duniani mpaka sasa.
"Hofu ya majanga ya magonjwa yanayoweza kuiangamiza dunia mara moja ni kubwa sana," anasema Joseph Miller, mwandishi mwenza (akishirikiana na Ken Miller) wa kitabu cha "Biology" (Prentice Hall, 2010).
"Hofu ya majanga ya magonjwa yanayoweza kuiangamiza dunia mara moja ni kubwa sana," anasema Joseph Miller, mwandishi mwenza (akishirikiana na Ken Miller) wa kitabu cha "Biology" (Prentice Hall, 2010).
Majanga ya kujitakia
Magonjwa ya asili siyo pekee yanayoweza kuleta hofu duniani. Mwaka
2011, jamii ya wanasayansi ilipagawa baada ya kugundua kwamba watafiti walikuwa
wametengeneza kirusi kipya cha mafua ya ndege kijulikanacho kama H5N1 ambacho
kilikuwa kinasambaa kupitia njia ya hewa.
Matokeo hayo yalizua taharuki duniani baada ya kubaini kwamba
magonjwa ya kutisha ambayo ni ya kutengenezwa yangeweza kusambaa kutoka kwenye
maabara za utafiti au yangeachiliwa kwa makusudi kabisa, na kusababisha janga
la dunia.
Kuvu (Fungus) miongoni
mwetu
Japokuwa bakteria ni hatari, lakini majanga ya kuvu (fungus)
ni hatari zaidi, anasema David Wake, mhifadhi katika Makumbusho ya Wanyama na
Wadudu (Museum of Vertebrate Zoology) katika Chuo Kikuu cha California,
Berkeley.
"Tumekumbana na ugonjwa mpya wa fangasi unaowashambulia
wanyama wa jamii ya amfibia ambao una madhara ya kutisha," alisema Wake akizungumzia
fangasi wa aina ya chytrid ambao
wanaua chura wengine nchini Marekani.
Ni wazi kwamba akitokea fangasi mwingine wa kutisha kwa
binadamu yatakuwa ni majanga. Na japokuwa bakteria ni hatari, kuna dawa za
kutosha kukabiliana nao. Kwa ulinganisho, hatufahamu sana kuhusu kutibu
magonjwa yanayosababishwa na fangasi kuliko ambavyo tunafahamu magonjwa
yanayosababishwa na bakteria, alisema Wake.
Vita vya Nyuklia
Mataifa mengi hivi sasa yanakusanya malighafi mbalimbali za
kutengeneza silaha za maangamizi, hasa za nyuklia. Ingawa mengi kati ya mataifa
hayo yamekuwa yakikanusha hadharani katika vikao vya usalama duniani, lakini
bado ukweli uko pale pale kwamba yanatengeneza silaha hizo na yamezificha, huku
yakiendelea kutafuta malighafi kila pembe ya dunia, hasa madini ya uranium.
Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo hivi sasa zinachimbwa
uranium na kampuni inayochimba inamilikiwa na serikali ya Urusi, ambayo kwa
miaka mingi inafahamika kwamba iko imara kijeshi na inaendelea kufanya tafiti
za silaha mbalimbali.
Kwa hiyo, wanasayansi wana hofu kubwa kuhusu tishio la mwisho
wa dunia: hasa vita ya dunia ya nyuklia. Fikiria kama hivi sasa tu wapo watu
wanaovaa mabomu ya kujitoa muhanga na kufanya ugaidi, je, akitokea mwendawazimu
mmoja akaamua kuyafurumua mabomu ya nyuklia ili ‘tufe wote’ maana yake ataifuta
dunia.
Ukiacha jitihada za silaha kali za Kim Jong Un wa Korea
Kaskazini pamoja na silaha za nyuklia za Iran, kuwepo kwa viwanda vingi vya
nyuklia duniani kunaweza kuisambaratisha dunia kama silaha hizo zitatua kwenye
mikono ya mwendawazimu mmoja.
Kiama kinaweza kufika kutokana na silaha za nyuklia au silaha
za kibaolojia au mabadiliko ya tabianchi.
Ujio wa maroboti
Filamu ya "The Terminator" iliyochezwa na Arnold Schwarzenegger
inaweza kuwa ni ubunifu tu wa kisayansi, lakini mashine na mitambo ya mauaji isiyoendeshwa
na watu inaweza kuwa karibu na uhalisia.
Miaka kadhaa iliyopita Umoja wa Mataifa ulipiga marufuku
matumizi ya maroboti ya mauaji — inawezekana hiyo ilitokana na ukweli kwamba
wataalamu wanahofia kuwa njia nyingi zimekuwa zikiyatengeneza.
Wanasayansi wa kompyuta wanafikiria kuhusu kukaribia kwa ‘umoja’
(singularity), mahali ambapo uwezo wa kufikiri wa kutengeneza, yaani artificial
intelligence, utazidi uwezo wa kibinadamu.
Kama maroboti hayo yatakuwa muhimu katika kusaidia au
yataharibu uwepo wa binadamu ni suala ambalo linahitaji mjadala. Lakini mambo
mengi yatakwenda kombo ikiwa yatakuwepo maroboti yenye uwezo mkubwa kuliko
binadamu yakiwa yametengenezwa kama silaha za mauaji ambayo yataiongoza dunia.
Ongezeko la watu
Hofu ya ongezeko kubwa la watu duniani limeonekana kuanzia
karne ya 18, wakati Thomas Malthus alipotabiri kwamba kuongeza kwa watu
kutasababisha njaa na kuijaza dunia.
Huku idadi ya watu duniani ikiwa bilioni 7 na ikiendelea
kupanda kwa kasi ya ajabu, wahifadhi wengi wanadhani kwamba ongezeko la watu ni
mojawapo ya majanga ya dunia.
Ni wazi, kwamba siyo kila mtu anakubaliana: Wengi wanadhani
ongezeko la watu linaweza kutengemaa katika miaka 50 ijayo, na kwamba wanadamu
watarekebisha madhara yake yanayotokana na wingi wa watu kwa sasa.
Madhara ya barafu
Pamoja ma matukio haya kwamba yatatokea, wanasayanasi wengi
wanadhani kwamba madhara ya mabonge ya barafu yanaweza kutokea, anasema Miller.
Kwa mfano, ongezeko la joto litaongeza athari za mazingira. Wakati
huo huo, mfumo wa ikolojia utaporomoka na kufanya iwe vigumu kuzalisha chakula,
huku nyuki wakiwa wametoweka kabisa duniani kutokana na kutokuwepo kwa miti
kwani ndio pekee wanaoweza kuchavusha mazao.
Kwa hiyo, badala ya madhara madogo, kuna sababu nyingine ndogo
ndogo ambazo zinaweza kuathiri maisha ndani ya Dunia mpaka pale wanadamu
watakapotambua hatari hiyo na kuibadilisha, kwa kurejesha hali ya misitu na
mazingira kwa ujumla.
chanzo: http://maendeleovijijini.blogspot.com

0 comments: