MFAHAMU MWENYEKITI MPYA WA UEFA

...................

Aleksander Ceferin ndie mwenyekiti mpya wa UEFA

Aleksander Ceferin ndio mwenyekiti mpya wa shirikisho la mpira wa migu Barani Ulaya (UEFA)


Aleksander Ceferin ndie mwenyekiti mpya wa UEFA
Mwenyekiti wa shirikisho la mpira wa migu la nchini Solvenia Aleksander Ceferin ndio mwenyekiti mpya wa UEFA baada ya kuibuka mshindi dhidi ya mpinzani wake mwenyekiti wa shirikisho la mpira wa migu la Uholanzi Michael van Praag.
Uchaguzi huo  walishiriki wanachama 55 wanao wakilisha nchi zao katika UEFA ambapo Aleksander Ceferin aliibuka mshindi kwa kura 42 dhidi ya mpinzani wake Michael van Praag ambae alipata kura 13.
Uchaguzi huyo ulifanyika mjini Athens nchini Ugiriki.
Baada ya kuibuka na ushindi huo Ceferin alizitoa shukurani kwa walio mpigia kura na kumalizia ya kwamba ushindi huo utaipa sifa Slovenia.
Ama kwa upande wake van Praag nae alizitoa shukurani kwa waliopigia kura huku akipongeza mgombea mwenza na ku ahidi hivi sasa wanaenda kuitengeneza UEFA mpya


chanzo: http://www.trt.net.tr
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: