KUTOKA UGANDA:Bunge la Uganda kutumia Dola 177,000 kuwatuza wabunge medali
Lango la kuingilia Bunge la Uganda jijini Kampalaiduwatochom
Bunge
nchini Uganda linatarajiwa kutumia Dola za Marekani 177,000 kuwatuza
medali wabunge 1,200 waliohudumu katika bunge la nchi hiyo kati ya mwaka
1962 hadi 2012.
Vyombo vya
Habari nchini humo vinaripoti kuwa sherehe za kuwatuza wabunge hao
zitafanyika mwishoni mwa mwezi huu katika maadhimisho ya miaka 50 ya
bunge hilo.
Kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye na mkewe Winnie Byanyima ni miongoni mwa wabunge wa zamani watakaopata medali hizo.
Raia wa Uganda, wameonekana wakipinga matumizi ya fedha hizo katika sherehe hizo wakati huu raia wa nchi hiyo wakiendelea kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi.
Hatua hii imekuja baada ya Gazeti la serikali ya New Vision kutangaza kuwa bunge limepanga kutumia fedha hizo kufanikisha shughuli hiyo.
Wabunge 13 wamefariki dunia kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
chanzo: http://sw.rfi.fr
Kiongozi wa upinzani nchini humo Kizza Besigye na mkewe Winnie Byanyima ni miongoni mwa wabunge wa zamani watakaopata medali hizo.
Raia wa Uganda, wameonekana wakipinga matumizi ya fedha hizo katika sherehe hizo wakati huu raia wa nchi hiyo wakiendelea kukabiliana na hali ngumu ya kiuchumi.
Hatua hii imekuja baada ya Gazeti la serikali ya New Vision kutangaza kuwa bunge limepanga kutumia fedha hizo kufanikisha shughuli hiyo.
Wabunge 13 wamefariki dunia kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita.
chanzo: http://sw.rfi.fr
0 comments: