WATUMIAJI WA MTANDAO WA YAHOO MNALIFAHAMU HILI....?

...................

Hofu kwa watumiaji wa mtandao wa Yahoo baada ya taarifa za wateja wake milioni 500 kuibiwa


mediaKampuni ya Yahoo imesema taarifa za wateja wake milioni 500 zimeibiwa na maharamia wa mtandao kwa ufadhili wa Serikali.REUTERS/Denis Balibouse/File Photo
Kampuni ya mtandao wa Yahoo, inasema kuwa udokozi wa taarifa za wateja wake zaidi ya milioni 500 duniani, ulikuwa ni mpango uliofadhiliwa na Serikali, wizi ambao ni mkubwa zaidi kuwahi kufanyika katika historia ya uharamia wa kimtandao.
Wizi huu umehusu taarifa binafsi za watu, ikiwemo majina na barua pepe, pamoja na maswali ya kiusalama ambayo mtu huyatumia kwaajili ya kuthibitisha akaunti yake.
Uharamia huu wa taarifa ulifanyika mwaka 2014 lakini taarifa hizo zimewekwa wazi mwaka huu.
Tayari shirika la ujasusi la nchini Marekani FBI limesema limeanza kuchunguza tukio hili.
Yahoo imesema kuwa “taarifa zilizoibiwa ni pamoja na majina, anuani za barua pepe (emails), namba za simu, tarehe za kuzaliwa, nywila (passwords), lakini sio taarifa za benki,” ilisema taarifa ya Yahoo.

End of break ads in 22s
Publicite, fin dans 22 secondes
Yahoo imesema kuwa, taarifa hizi “ziliibiwa na kile kinachoaminika kuwa ni ufadhili wa Serikali” huku ikishindwa kuweka wazi ni nchi gani ambayo imehusika kwenye tukio hili.
Habari za kuwepo kwa tukio la uharamia wa taarifa za kampuni hii ya masuala ya teknolojia, zilianza kuvuma mwezi Agosti mwaka huu, pale maharamia wanaofahamika kwa jina la “Peace” walipokuwa wakijaribu kuuza taarifa za watumiaji milioni 200 wa Yahoo.
Alhamisi ya juma hiki Yahoo ilisema kuwa, taarifa zilizoibiwa ni nyingi kuliko vile walivyokuwa wakibashiri hapo awali.
Nchini Uingereza, kampuni ya ISP Sky na BT wametoa onyo kwa wateja wao kuwa wanaweza kuathirika kutokana na wizi huu, ambapo Yahoo ni mtoa huduma namba moja kwa makampuni hayo, na kuwataka wateja wake wabadili Passwords zao

chanzo: http://sw.rfi.fr/
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: