Unaufahamu wimbo utakaotumika kama kitambulisho kombe la dunia?

...................

Wimbo wa Stevie Wonder ni kitambulisho


BBC Kutumia nyimbo za Stevie Wonder kama kitambulisho
Wimbo wake Stevie Wonder, Another Star, utakuwa wimbo utakaopeana sauti mrejeo katika maonyesho ya BBC ya kombe la dunia.
Wimbo huo, pamoja na ule wa Kilatino , zitatumika kama nyimbo za kufungua vipindi vyote vya Kombe la Dunia Brazili 2014, vitakavyopeperushwa kupitia BBC.
Nndio mara ya kwanza kabisa kwa mwanamziki huyu, mwenye uri wa miaka 64, kukubali wimbo wake utumike katika namna hii.
BBC kupeperusha mechi za WC_2014 moja kwa moja
Wonder aliutoa wimbo huo kiasili, katika mwaka wa 1976, kwenye albamu yake iliyoshinda tuzo la Grammy mara nyingi, iitwayo Songs in the Key of Life.
Wimbo huo, kwa mara ya kwanza utachezwa kwenye kituo cha BBC One tarehe 11, Juni, saa ili kukitambulisha kipindi kinachoangazia kipute hicho cha kombe la dunia.
Mtayarishi mkuu wa kitengo cha michezo, BBC, Ian Finch alisema kuwa BBC ilikua yenye bahati kupewa ruhusa ya kutumia wimbo huo.
‘Wimbo huu unaonyesha kwa uzuri hisia za sherehe na furaha ambazo tutawaletea watazamaji wetu katika msimu huu wa kombe la dunia.’ Finch.
BBC Kutumia nyimbo za Stevie Wonder kama kitambulisho
BBC itaonyesha kwa kina Kombe la Dunia.
Itaonyesha michuano ya moja kwa moja katika BBC One, BBC One HD na tovuti ya BBC Sport na BBCSwahili.
Michuano mingine itakua ikiendelea katika BBC Three, BBC Three HD na Red Button.
BBC Two na BBC Two HD zitaonyesha mchuano huo kwa kifupi masaa ya asubuhi, na pia marudio ya mchuano wote .

source:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: