Paka mkubwa aonekana Paris

...................



Buka mdogo
Polisi nchini Ufaransa,askari wa zima moto na polisi waliopewa mafunzo maalum ya kikosi cha mbwa wako katika msako mkubwa wa kumtafuta paka mkubwa aliyeingia mjini.
Paka huyo mkubwa anaaminika kuwa ni chui mkubwa mwenye mistari kama ya pundamilia maarufu kama buka,alionekana katika moja ya maduka makubwa na hata kwenye maegesho ya magari mjini Paris.
Chopa inaongezea nguvu katika harakati za kumsaka buka huyo ndani na nje ya mji wa Montevrain.Polisi wamewataka raia wa mji huo na mingine miwili wasitoke nje ya nyumba zao ama matembezi ya jioni wakati wa zoezi la kumsaka Buka huyo.
Wazazi wamesha chukua watoto wao mashuleni kwa magari baada ya taarifa za kuonekana Buka huyo mjini bustanini.

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: