Besigye apinga matokeo ya uchaguzi Uganda

...................
,


Mmoja wa wapinzani wakuu katika uchaguzi mkuu uliomalizika hivi punde nchini Uganda, Dkt Kizza Besigye, amekatalia mbali matokeo ya uchaguzi huo, uliofanyika siku ya Alhamisi.
Bw Besigye ambaye amekuwa akizuiliwa nyumbani kwake tangu siku ya Ijumaa amesema kuwa raia nchini Uganda wameshuhudia ulaghai mkubwa mno wa uchaguzi mkuu, kuwahi kufanyika katika taifa hilo la mashariki mwa Afrika.
Kanali huyo mstaafu ameelezea uchaguzi huo kama usio halali na kuwa ni mapinduzi ya kijeshi.
Rais wa muda mrefu Yoweri Kaguta Museveni, alitangazwa mshindi.

ZAIDI BOFYA HAPA CHINI: 

http://www.bbc.com

http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: