Papa Francis awapa pole wa Kenya

...................
 
Papa Francis akiwasalimia waumini wakatoliki,wakati wa sikukuu ya Pasaka. 
 
Katika maadhimisho ya ibada ya sikukuu ya Pasaka, baada ya mateso,kifo na ufufuko wa Yesu Kristo,Baba Mtakatifu Francis amewaombea wanafunzi waliouawa nchini Kenya mwishoni mwa wiki iliyopita.
Katika utaratibu wake wa kawaida wa kutoa ujumbe katika sikukuu ya pasaka,akizungumza na umati wa waumini waliofurika katika viwanja vya Basilica ya Mtakatifu Peter mjini Vatican, Papa ametoa mwito wa kusitisha kile alichokiita matukio mengi ya mateso ya wakristo ulimwenguni.
Kiongozi huyo wa kiroho anayeongoza waumini wa madhehebu ya kikatoliki wapatao bilioni moja nukta mbili ,amelaani mgogoro unaondelea Mashariki ya kati na kwingineko, lakini ameweka imani yake katika mazungumzo yanayoendelea juu ya mkataba wa vinu vya nyukilia vya Irani ,wenye mwanga wa matumaini wa kufikiwa makubaliano na kuifanya dunia kuwa mahali salama pa kuishi.
Kabla ya kuanza hotuba yake,Papa alikwenda katika viwanja hivyo vya Basilica la Mtakatifu Petro kuwasalimia waumini waliokuwa wakimsubiri pamoja na kwamba kulikuwa na hali mbaya ya hewa.

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: