Mbwa ‘shujaa wa Paris’ avuma mtandaoni

...................


Image caption Diesel aliuawa kwenye operesheni ya polisi mtaa wa Saint Denis Jumatano
Katika vita, huwa kuna watu wanaoibuka mashujaa na kuenziwa na watu na taifa kwa jumla.
Huko Ufaransa, kuna mbwa mmoja wa polisi ambaye amepata umaarufu mkubwa sana na kusifiwa baada yake kufariki kwenye operesheni ya polisi.
Mbwa huyo wa jina Diesel anaweza kuelezwa kuwa ‘afisa wa polisi’ wa kwanza kufa vitani katika operesheni dhidi ya washukiwa walioshambulia Paris Ijumaa.
 
Mtandaoni, kulianzishwa kitambulisha mada, "Je Suis Chien," (Mimi ni Mbwa) ambacho kinafuata kitambulisha mada cha "Je Suis Charlie" ambacho watu walitumia kuonyesha uungaji mkono wao kwa jarida la Charlie Hebdo kufuatia shambulio jingine mapema mwaka huu.
Kuna hata ukurasa uliofunguliwa kwenye Twitter wenye jina lake na mada hiyo 'Je Suis Chien'
 
Kitambulisha mada hicho kimesambazwa zaidi ya mara 50,000, wengi wakiandika hivyo kwa Kifaransa na baadaye kwa Kiingereza.
Kwenye Twitter, habari za kuuawa kwa mbwa huyo wa umri wa miaka saba na "magaidi” zilisambazwa zaidi ya mara 13,000.
"Twashukuru sana viumbe kama hawa,” aliandika mmoja wa watu.
Aliyeanzisha kitambulisha mada hicho anasema alikuwa akifanya mzaha tu.
Ashley, 24 anayeishi karibu na Paris alisema: “Nilitaka kuwe na mzaha kiasi kwa sababu tovuti karibu zote zilikuwa zinazungumzia hili”.
Aliambia BBC Trending kwamba alianzisha kitambulisha mada hichi ili pia kufanyia mzaha kuenea kwa vitambulisha mada vya"Je Suis...". "Kila tatizo likitokea kuna #JeSuis," amesema.
 
"Shujaa halisi, alifariki leo kwa ajili ya uhuru wako kesho"
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: