TOKA MLOWO-SONGWE:Polisi yataka kususiwa chakula cha msibani

...................

kamanda wa polisi mkoa wa songwe akiongea na wananchi kutatua mgogoro huo
Na Saimeni Mgalula,Songwe
Hali ya uvunjifu wa amani ilitanda katika mji mdogo wa mlowo wilayani Mbozi Mkoani songwe,Baada ya wananchi kuchoma moto magurudumu ya magari katika barabara itokayo mkoa wa Mbeya kwenda Tunduma mkoani hapa.
Tukio hilo la kusikitisha  lilitokea majira ya mchana Agost 28 mwaka huu baada ya wananchi wa Mlowo kudai kuwa mkazi mmoja aliyefahamika kwa jina la Stanslaus Kalinga (42) kupigwa na Askari baada ya kukamatwa kwa kosa la uzembe na uzururaji. Marehemu alifia katika hospitali ya Wilaya ya Mbozi akipatiwa matibabu.
Naye Diwani wa Kata ya Mlowo Sebastian Kilindu alikiri kutokea kwa tukio hilo na baadaye alikwenda Polisi ili kupata ukweli wa tukio hilo kuwa je ni kweli polisi wamejihusisha na tukio hilo ili aweze kubaini ukweli huo.ambapo aliambiwa askari hawajajihusisha na tukio hilo.
Akithibitisha tukio hilo kamanda wa polisi mkoa wa songwe Mathias Nyange alisema kuwa jeshi la polisi lilimkamata marehemu huyo na hakupigwa na polisi kama inavyodaiwa kwani taarifa kamili juu ya kifo hivyo nitaitoa baada ya uchunguzi wa Daktari
Katika hali isiyo ya kawaida wakazi wa Mlowo walibeba chakula kutoka msibani na kukipeleka kituo cha Polisi Mlowo wakiwa hawana ukeli wa kifo cha marehemu ambacho kilisababishwa na Askari hivyo nao washiriki kula chakula hicho.
Hali iliyopelekea polisi kutumia mabovu ya machozi ili kuwatawanya  wananchi hao . Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Mlowo alimuomba Kamanda wa Polisi Mkoani Songwe kufanya suluhu na wananchi hao kwa kuwa Askari hawana kambi wanaishi nao mitaani hivyo mgogoro huo utatuliwe kwa amani na sio kitofauti.

 
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: