RAIS WA ZIMBABWE: MAJAJI WAMEFANYA UZEMBE KURUHUSU MAANDAMANO YA UPINZANI

...................
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe amewatuhumu majaji wa mahakama za nchi hiyo kuwa wazembe kwa kuruhusu maandamano ya kupinga serikali ambayo baadaye yaligeuka kuwa ya fujo na machafuko.
Mugabe alitoa matamshi hayo jana katika mkutano wa tawi la vijana la chama tawala cha ZANU-PF, siku mbili kabla ya Mahakama Kuu kusikiliza shauri la kupinga uamuzi uliotolewa wiki iliyopita wa kupiga marufuku rasmi maandamano ya upinzani.
Serikali ya Zimbabwe ilichukua uamuzi wa kupiga marufuku kwa muda wa wiki mbili maandamano yote katika mji mkuu Harare ambao umekuwa ukishuhudia maandamano ya kulalamikia utendaji wa Rais Mugabe katika kushughulikia matatizo ya uchumi, uhaba wa fedha na ukosefu wa ajira nchini humo.
Maandamano ya kulalamikia utendaji wa Mugabe
Kwa mujibu wa toleo la leo la gazeti la Sunday Mail, Rais Mugabe aliuambia mkutano huo wa vijana wa chama chake tawala kuwa "hawezi kuvumilia tena" na kwamba hatoruhusu maandamano ya fujo na machafuko yaendelee kufanyika.
Kwa mujibu wa gazeti hilo Mugabe amesema mahakama, mfumo wa sheria na majaji wa Zimbabwe wanapaswa kuwa watu wenye uelewa zaidi kuliko raia wa kawaida na kwamba wasizembee katika maamuzi wanayotoa wakati yanapowasilishwa maombi na watu wanaotaka kuandamana.
Rais Robert Mugabe
Kufuatia kauli hiyo ya Rais Mugabe, kiongozi wa chama cha Kidemokrasia cha Wananchi, Tendai Biti na ambaye pia ni mwanasheria aliyeongoza mpango wa kuwasilisha shauri la kupinga marufuku ya maandamano iliyotangazwa hivi karibuni, amemtuhumu Mugabe kuwa anatoa vitisho dhidi ya mahakama na kukiuka katiba.
Tendai Biti, kiongozi wa upinzani
Wakiongozwa na Biti, wanaharakati kadhaa wa kisiasa wamewasilisha shauri katika Mahakama Kuu kupinga uamuzi huo wa serikali wakisema kuwa ni kinyume na Katiba. Shauri hilo linatazamiwa kusikilizwa hapo kesho
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: