VIDEO: Kondomu inavyotumika kufukuza wanyama Tarangire Arusha

...................

Shirika la HoneyGuide Arusha  kwa kushirikiana na wananchi wa maeneo jirani na mbuga ya Tarangire walibuni njia ya kufukuza wanyama ili wasiharibu mazao yao na kuwafukuza mbali na makazi yao. 
Unaambiwa wamekuwa wakitumia Kondomu kuzuia wanyama kama tembo kuharibu mazao. Imeelezwa kuwa wanatumia mchanganyiko wa baruti ya pilipili na kondomu kufukuza wanyama waharibifu. Mchanganyiko huo ukitupwa hewani Tembo wanapofikiwa na ile  harufu ya pilipili ukimbia au kusogea mbali zaidi.
Njia hii imeelezwa kufanya kazi vizuri na pia imekuwa ikisaidia wanyama kutopata madhara.mkuu wa kitengo cha mawasiliano kutoka shirika la HoneyGuide, Ng’orongo Nyamoni Ng’orongo ambaye ameeleza namna wanavyotumia Kondomu kufukuza wanyama………
>>>’Tumetumia kondomu kama tu kiwezeshaji cha kuweza kubeba mchanganyiko kati ya mchanga na hiyo pilipili na kwa sababu kondomu inayeyuka haraka na kulipuka kwa urahisi’

chanzo: http://millardayo.com
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: