DARASA ASEMA...ETI AMEWAHI KWENDA KWA MGANGA WA KIENYEJI: KILICHOMPELEKA HIKI HAPA (VIDEO)

...................
Msanii wa bongofleva Darassa ambaye jina lake limeongoza kwa kutajwa mara nyingi kwenye namba kubwa za chati za Radio/TV Tanzania kutokana na hit single ya ‘muziki‘ amekaa kwenye Exclusive Interview na Diva kwenye Ala za Roho CloudsFM.
Diva amemuuliza Darassa maswali mbalimbali ikiwemo ya maisha yake ya kimapenzi na maisha ya mtaani kwa ujumla ambapo Darassa amekiri kwamba aliwahi kwenda kwa mganga wa kienyeji ili kutafuta suluhisho la maisha aliyokua anayapitia.
Amesema ‘Nimeshawahi kwenda mganga zamani sana, ni miaka imepita na sababu ya kwenda haikuhusiana na muziki bali maisha yangu binafsi, kwenye maisha ya uswahilini ni vitu vingi vinatokea na ilikua ni ushawishi wa watu wengine…. sikupewa dawa wala sikuchanjwa taratibu za mganga zilinifanya nisifikie huko‘
Kwenye akili ya kujitambua unaambiwa vitu vingi kama kijana au mtu anaetafuta maisha unaweza ukachanganywa na vitu vingi sana lakini nakwambia Mungu ni wa ajabu sana, miaka ambayo nilikwenda kwa Mganga nilikua bado sijaiachia ‘sikati tamaa’ na sikuwahi kufanikiwa‘ – Darassa

Hapa ni video ya mazungumzo na mwandishi
.
chanzo:milardayo.com

http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: