Waachiliwa kuhusu kosa la fidia Libya

...................
Mabaki ya ndege iliyolipuliwa katika shambulizi la Lockerbie

Maafisa wawili, wa Libya wameachiliwa, katika kesi iliyokuwa inawakabili ya kufuja pesa za umma kwa kukubali kuwalipa fidia waathiriwa wa shambulizi la ndege katika anga ya Lockerbie mwaka 1988.
Kesi dhidi ya waziri wa zamani wa mambo ya nje Abdelaaty al-Obeidi na mkuu wa baraza la Congress Mohamed al-Zway wamekuwa ,imekuwa ikisikilizwa tangu mwaka 2012.
Rais wa zamani wa Libya, kanali Muammar Gaddafi alikubali kuwalipa fidia waathiriwa mwaka 2003.
Hii ndiyo hukumu ya kwanza kutolewa dhidi ya maafisa wakuu tangu kuuawa kwa Gadaffi.
Jaji hakuelezea sababu za kuwaachilia huru wawili hao , kulingana na mwandishi wa BBC Rana Jawad mjini Tripoli.
Mmoja wa jamaa za al-Zway, aliambia BBC kuwa hii ni ishara tosha kwamba Libya ina mfumo huru wa kisheria.
''Nina furaha sana na idara ya mahakama kuwa nilikuwepo wakati hukumu ikitolewa,'' alisema jamaa huyo.

chanzo:bbc swahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: