Mapendekezo 9 ya Wazanzibar

...................

Kamati ya Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar inayoongozwa na mwanasiasa mkongwe, Mzee Hassan Nassor Moyo, imeyataja mambo tisa ambayo yanastahili kujumuishwa katika katiba mpya ili kuondosha malalamiko ndani ya muungano.
Makamo wa rais Seif Sharif Hamad na rais Dr.Ali Mohamed Shein
Wakati Rasimu ya Katiba mpya ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania ikitarajiwa kutangazwa wakati wowote mwezi ujao, Kamati ya Maridhiano ya Kisiasa Zanzibar inayoongozwa na mwanasiasa mkongwe, Mzee Hassan Nassor Moyo, imeyataja mambo tisa ambayo yanastahili kujumuishwa katika katiba mpya ili kuondosha malalamiko ndani ya muungano. Mambo hayo ni pamoja na jina la Jamhuri ya Tanzania kuwa Jamhuri za Tanzania, ufafanuzi kuhusu jeshi la Polisi; maliasili ya mafuta na gesi asilia, suala la sarafu, miongoni mwa mambo mengine. Kusikiliza mahojiano ya Sudi Mnette na Naibu wa Katibu wa Kamati hiyo ya Maridhiano, Eddy Riamy, bonyeza alama ya kusikiliza masikioni hapo chini.
Mwandishi: Sudi Mnette
Mhariri: Mohammed Khelef

chanzo:dw swahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: