WAMAREKANI WEUSI WAWEKA HISTORIA

...................


Barack Obama azindua jumba la makumbusho ya histoira ya raia wa Marekani wenye asili ya Afrika


Jumba la makumbusho ya historia ya wamarekani weusi lazinduliwa

 

Rais wa Marekani Barack Obama amezindua Jumamosi jumba la makumbusho ya historia ya raia wa Marekani wenye asili ya Afrika Septemba 24 mjini Washington.

Katika hafla hiyo ya uzinduzi wa jumba hilo la makumbusho, watu takriban 7 000 walihudhuria katika hafla hiyo kutoka katika maeneo tofauti nchini Marekani.
Tukio hilo litaacha athari kubwa katika historia kwa kuwa Barack Obama ni rais wa kwanza mwenye asili ya Afrika kuongoza nchi.
Jumba hilo la makumbusho lililkuwa likiombwa na jamii ya wamarekani wenye asili ya Afrika tangu mwaka 1950 na ujenzi wake kuruhusiwa na rais George Bush mwaka 2003.
Mwanamuziki kutoka Afrika Magharibi kwa jina la Angelique Kidjo alifungua tamasha hilo kwa kutumbiza akifuatiwa na Stevie Wonder na PattiLaBelle.
Katika hotuba yake rais Obama alifahamisha kuwa jamii ya wamarekani wenye asili ya Afrika walichangia kwa kiasi kikubwa  ujenzi wa Marekani
 
chanzo: http://www.trt.net.tr
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: