Unawafahamu Wachezaji watano wa kuchungwa kwenye kikosi cha Azam FC msimu wa 2015/16?

...................

Wachezaji watano wa kuchungwa kwenye kikosi cha Azam FC msimu wa 2015/16


Goal inakuletea wachezaji watano wa kuchungwa kwenye kikosi cha Azam FC msimu huu 2015/16
1.Farid Mussa Maliki
Chipukizi mwenye thamani ya Tsh. Milioni 20 aliyepo kwenye kikosi cha kwanza cha kocha Stewart Hall ambaye baada ya kuandamwa na majeruhi ya muda mrefu msimu huu ameonekana kuwa na kasi ya ajabu na kutarajiwa kuwa na mchango mkubwa kwenye timu hiyo.
Baada ya kufanya vizuri kwenye michuano ya Kombe la Kagame ikiwepo bao lake zuri kwenye mchezo wa nusu fainali dhidi ya KCCA, ya Uganda na kufanya vizuri kwenye pambano la Ngao ya Jamii dhid I ya Yanga Maliki ameonyesha kuwa ni mchezaji wa kuchungwa na atakuwa na msaada mkubwa kwa kikosi cha Azam msimu huu.
2.John Bocco
John Bocco mshambuliaji kipenzi cha kocha Stewart Hall wa Azam amekuwa kwenye kiwango cha juu hivi sasa na ni mmoja ya wachezaji hatari na ghali walipo kwenye kikosi cha mabingw hao wa Kombe la Kagame.
Bocco anahitaji kuwekewa ulinzi mkali na mabeki wa timu pinzani kutokana na mshambuliaji huyu mrefu kulijia vuzri goli kila anapopata nafasi ya kuweza kufunga uwezo aliouonyesha kwenye michuano ya Kombe la Kagame niwazi anaonekana kuwa na mchango mkubwa kwenye timu yake pindi ligi ya Vodacom itakapoanza hivi karibuni.


3.Kipre Tchetche
Mshambuliaji hatari wa Azam FC inatarajiwa kuwa na mchango mkubwa kwa timu yake kwenye msimu unaokuja wa 2015/16 kutokana na kurudi kwenye kiwango chake baada ya kuuguza majeruhi ya muda mrefu kitu kilichomfanya afanye vibaya msimu uliopita.
Tchetche raia wa Ivory Coast anafanya vizuri kwenye mechi mbalimbali za kirafiki na kuisaidia timu hiyo kupata matokeo mazuri na kurudi kwa kocha Stewart Hall kunaweza kumfanya mchezaji huyo akarududia rekodi yake ya kuwa mfungaji bora kama alivyofanya misimu mitatu iliyopita.


4.Allan Wanga
Bado hajaichezea timu hiyo hata mechi moja lakini ni mmoja ya washambuliaji anayetarajia kupewa ulinzi mkali na mabeki wa timu pinzani kutokana na uwezo wake mkubwa wa kufunga mabao kutokana na uwezo na nguvu alizokuwa nazo.
Wanga ametua Azam mwezi uliopita akisaini mkataba wa mwaka moja baada ya kuachana na El Merreikh ya Sudan aliyoichezea kwa mafanikio akitokea klabu ya FC Leopard ya kwao Kenya.
5.Mudathir Yahya
Huyu ni chipukzi mwengine anayetarajiwa kufanya mambo makubwa akiwa na kikosi cha Azam FC msimu ujao kutokana na kipaji alichokionyesha misimu miwili iliyopita na sasa kocha Stewart Hall ameonekana kumuamini na kumpa nafasi kwenye kikosi cha kwanza.
Muda alifanya vizuri kwenye michuano ya Kombe la Kagame na kuwaweka benchi wakongwe wengi akiwepo Didier Kavumbagu na Amme Ali

chanzo:goal.com
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: