UMEIPATA HII.. REFA APEWA KADI NYEKUNDU

...................

Mchezaji amwonesha refa kadi nyekundu Uturuki

 Salih

Salih Dursun alionesha refa kadi nyekundu
Mchezaji wa klabu ya Trabzonspor, Salih Dursun, alitolewa nje kwa kumuonyesha mwamuzi kadi nyekundu wakati wa mchezo waliofungwa mabao 2-1 na Galatasaray katika mchezo wa Ligi Kuu ya Uturuki.
Tukio hilo lilitokea dakika ya 86 ya mchezo, klabu hizo zikiwa zimetoshana nguvu 1-1, baada ya mwamuzi Denis Bitnel kumuonyesha kadi nyekundu ya moja kwa moja Luis Cavanda kwa kufanya madhambi ndani ya eneo la hatari. Aidha, aliwazawadi Galatasaray penalti.
Trabzonspor walikuwa tayari wamesalia wachezaji tisa uwanjani kabla ya kutokea kwa kisa hicho.
Wachezaji wa Trabzospor walimzingira mwamuzi kupinga kadi hiyo.
Ni wakati huo ambapo Dursun alimnyang’anya refa kadi nyekundu aliyokuwa nayo na kumuonyesha kadi hiyo hatua ambayo ilipelekea na yeye kufukuzwa uwanjani.
  Trabzonspor
Wachezaji wa Trabzonspor wakifurahia kufunga bao awali
Hii sio mara ya kwanza kwa klabu hiyo kuingia katika mizozo na waamuzi, kwani Novemba mwaka jana mwenyekiti wao Ibrahim Haciosmanoglu alifungiwa siku 280 baada ya kuwafungia waamuzi wanne uwanjani kwa kushindwa kutoa penati kwa timu hiyo.

chanzo:bbcswahili
http://3.bp.blogspot.com/-e0QpO-QtZzE/U5DWDUZasXI/AAAAAAAABWg/QlFF97gwNdc/s1600/RAHA+GIF.gif
GIVE YOUR OPINIONS HERE

0 comments: